CONTACT US:

CONTACT US:
Mobile : 0755 484866
EMAIL : socialworkertz@yahoo.com

Monday, December 21, 2015

VIPIMO VYA VINASABA (DNA)

VINASABA (DNA) NI NINI?

Ndugu zangu

Watu wengi hasa wanaume wamekua wakiwakana mimba au watoto wao punde tu inapotokea migogoro kwenye mahusiano na wenzi wao.
Leo tupeane taarifa kidogo juu ya vipimo vya vinasaba.

Vipimo vya Nasaba ni nini?

Hivi ni vipimo ambavyo vinatoa ushahidi thabiti juu ya uzao wa mtoto. Baba anayedhaniwa kuwa baba mzazi anapimwa vipimo vya nasaba ili kuwa na uhakika kwamba yeye ndiye baba mzazi.

Nasaba hupatikana katika kiini cha seli hai na huwa na taarifa za urithi kutoka kwa mzazi kwenda kwa mtoto. Taarifa za nasaba ndizo pekee zenye kutoa ukweli usiopingika kuhusu uzao wa mtoto.

MAOMBI YA NASABA (DNA)

Kama baba wa mtoto hajulikani, nani anaweza kuomba uthibitisho wa uzao?

Wafuatao wanaweza kuomba amri ya kuthibitisha uzao wa mtoto: (a) Mtoto; (b) Mzazi wa mtoto; (c) Mlezi wa mtoto; (d) Ofisa wa Ustawi wa Jamii; au (e) Kwa ruhusa rasmi ya mahakama, mtu yeyote mwenye kuvutiwa na mtoto.

WAKATI GANI MAOMBI YANAWEZA KUFANYWA? (a) Kabla mtoto hajazaliwa; (b) Baada ya kifo cha baba au mama wa mtoto; (c) Kabla mtoto hajafikisha umri wa miaka kumi na nane. Inawezekana pia, kwa ruhusa rasmi ya mahakama, kuomba amri ya kuthibitisha uzao baada ya mtoto kufikisha umri wa miaka kumi na nane.

Mawasiliano
Simu: 0686 484866
Email: socialworkertz@yahoo.com

1 comment:

  1. Huyo Nai kaingije hapo, au huyo mtoto hana hakika nae?

    ReplyDelete