CONTACT US:

CONTACT US:
Mobile : 0755 484866
EMAIL : socialworkertz@yahoo.com

Tuesday, March 27, 2012

WIMBI LA UBAKAJI LABEBA SURA MPYA, ABAKA MTOTO WA MIAKA MIWILI – MBEYA.

Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya. Wimbi la ubakaji kwa watoto mkoani Mbeya limechukua sura mpya baada ya mkazi mmoja wa Kijiji cha Ikukwa, Wilaya ya Mbeya Vijijini kumbaka mtoto mwenye umri wa miaka miwili bila huruma. Tukio hilo limetokea majira ya saa 8 mchana Machi 24 mwaka huu, ambapo mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Manase (30) kumbaka mtoto baada ya kumrubuni mtoto na kwenda naye nyumbani kwake na kisha kufanyia ukatili huo. Baada ya kusikika kwa kelele chumbani kwa Manase, wananchi walifuatilia na kukuta mtoto akiwa amejeruhiwa vibaya , ambapo walimkamata mbakaji huyo na kumpeleka Kituo cha Polisi Kati kilichopo Jijini Mbeya . Hata hivyo mtuhumiwa anashikiliwa Kituoni hapo na Jeshi la Polisi na wakati wowote atafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.. Wakati huohuo mtoto aliyebakwa amelazwa katika Hospitali ya Rufaa iliyopo jijini hapa, akipatiwa na matibabu na uchunguzi wa kitendo hicho umebaini kuwa ni imani za kishirikiana.

No comments:

Post a Comment